Isaiah 42:23-25


23 aNi nani miongoni mwenu atakayesikiliza hili,
au atakayezingatia kwa makini katika wakati ujao?

24 bNi nani aliyemtoa Yakobo kuwa mateka,
na Israeli kwa wateka nyara?
Je, hakuwa yeye, Bwana,
ambaye tumetenda dhambi dhidi yake?
Kwa kuwa hawakufuata njia zake,
hawakutii sheria zake.

25 cHivyo akawamwagia hasira yake inayowaka,
ukali wa vita.
Iliwazunguka kwa miali ya moto, lakini hata hivyo hawakuelewa;
iliwateketeza, lakini hawakuyatia moyoni.
Copyright information for SwhKC